30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

ROSE NDAUKA: MSIWASAMEHE WANAOWANYANYASA KIMAPENZI

Rose Ndauka

 

 

Na KYALAA SEHEYE,

STAA wa filamu za bongo, Rose Ndauka, amewatahadharisha wanawake wenzake kwamba wasiwasamehe wanaume wanaowanyanyasa kimapenzi ndani ya nyumba zao, kwa kuwa kufanya hivyo ni kujinyima haki kisheria.

Rose alisema mwanamke anayejielewa hatakubali kunyanyasika awapo kwenye ndoa yake na anayeogopa ni yule asiyejitambua, bali anaishi ilimradi kaolewa.

“Huwa nachukizwa sana na mwanamke anayekubali kunyanyaswa katika ndoa na kujifanya mvumilivu, wakati karne hii mwanamke wa aina hiyo anadharaulika na jamii yote inayomzunguka kwa kuwa hatambui thamani yake,” alisema Rose Ndauka.

Rose aliongeza kwamba, wanawake wanaofichua manyanyaso wanayofanyiwa na wenzi wao huwa mashujaa na umma hujifunza kupitia kwao, badala ya kuficha na kuugulia ndani kwa ndani, huku ukiishia kuteketea moyoni ama kujiua.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles