30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

RC Mwanza azuia matukio yasiyo ya lazima yanayosababisha mikusanyiko

Na Clara Matimo, Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel, amepiga marufukj matukio yote yasiyo ya lazima yanayosababisha mikusanyiko lengo likiwa ni kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa corona.

Pia amewasisitiza  wakazi wa mkoa huo kufuatilia kwa makini elimu inayotolewa na wataalamu wa afya kuhusu  jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa corona.

Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake Julai 20, 2021, Mhandisi Gabriel amezitaka Mamlaka zinazohusika kutoa vibali vya mikusanyiko kusitisha katika kipindi hiki ambacho mkoa unaendelea kupambana ili  kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa corona.

“Mikusanyiko isiyokuwa na sababu yoyote hakuna sababu ya kutoa vibali  kipindi hiki  tuko kwenye kampeni ya kumlinda mwana Mwanza, usalama wa maisha kwanza, mengine yanakuja  baadaye.

 “Vikao vinakuja baadaye, mikutano inakuja baadaye,  siasa zinakuja baadaye na matamasha yanakuja baadaye lakini kwanza ni usalama wa maisha yetu,”alisisitiza.

Amesema matukio ambayo siyo ya lazima yanayosababisha mikusanyiko hayataruhusiwa kabisa ila ibada  ma misiba iendelee lakini kwa uangalizi wa hali ya juu.

“Nasisitiza wananchi kuvaa barakoa wanapokuwa kwenye mikusanyiko ya lazima kama nyumba za ibada na kwenye msiba pia kila mtu ahakikishe ananawa mikono ama atumie vitakasa mikono pamoja na kuhakikisha anakaa mbali na mtu mwingine tukitimiza hayo tutakuwa  tunaendelea kujilinda,” alisema na kuongeza;

“Katika mkoa etu tumetenga wiki moja kwa ajili ya kuuombea mkoa wetu Mwenyezi Mungu atuepushe na ugonjwa huo, kila mmoja kwa dini yake na kwa muda wake aombe kwelikweli maana Mungu ndiye tegemeo letu,” amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles