25.8 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

RC AKUTANA NA WADHIBITI ELIMU

Na Mwandishi Wetu, RUKWA

MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Zelote Stephen amekutana na wadhibiti ubora wa shule wa halmashauri nne za mkoa huo  kujua changamoto wanazokumbana nazo na mambo yanayosababisha kushuka kiwango cha elimu.

Stephen alifikia uamuzi huo baada ya  mkoa wake kushuka katika elimu kutoka nafasi ya 6 mwaka 2015 hadi nafasi ya 12 kati ya mikoa 31 mwaka 2016 katika  mtihani wa kidato cha nne.

Pia mkoa huo umeshuka katika mitihani ya kidato cha pili kutoka nafasi ya 20 kwa mwaka 2015 hadi nafasi ya 21  mwaka 2016.

Wadhibiti hao walielezea sababu nyingi  zilizosababisha kushuka   kiwango cha elimu, mojawapo ikiwa ni kutopewa mrejesho wa taarifa za kila wiki wanazoziandika na kukabidhi kwa wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya.

“Tangu Julai, mwaka jana tumeshaandika ripoti nyingi tu zinazoelezea upungufu kama vile walimu kwa baadhi ya masomo, matundu ya vyoo na vitabu vya kusomea,”alisema Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Goreth Ntulo.

Alisema sababu nyingine  zinazokwamisha ufanisi wa kazi za wadhibiti hao  ni kutopewa motisha na mwajiri wao na kusababisha waishi katika maisha magumu.

“Mimi sijawahi kwenda likizo kwa fedha ya Serikali tangu nianze kufanya kazi, na madaraja hatupandishwi…hata  ukipandishwa linabaki jina tu… mshahara upo pale pale,”alisema mmoja wa wadhibiti hao.

Akijibu hoja hizo, RC Stephen aliwaagiza wakurugenzi wote kuhakikisha  wadhibiti hao wanapatiwa mrejesho juu ya kasoro walizozibaini baada ya kufanya ukaguzi katika shule zao.

Mmoja wa wadhibiti hao, Pracida Rwegasira  alisema amefurahishwa na uamuzi wa kuitwa  kutoa mchango wao utakaosaidia kuinua kiwango cha elimu mkoani humo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles