24.7 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 19, 2024

Contact us: [email protected]

Rapa aliyetaka kujiua aomba radhi

LOS ANGELES, Marekani

MKALI wa muziki wa Hip hop nchini Marekani, Kodak Black, amewataka radhi mashabiki wake kwa kile alichosema anatamani kujiua kutokana na upweke na huzuni aliyonayo.

Sasa, rapa huyo mzaliwa wa Florida ametumia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter kutaka asamehewe kwa kauli hiyo.

Kwa upande wao, mashabiki wamepokea kwa mikono miwili msamaha huo, ambapo mmoja wao ameandika: “Endelea kukaza #KodakBlack, wewe ni rapa muhimu zaidi ya wote walioibuka katika miaka ya 2010…”

Kodak amekuwa akipamba vichwa vya habari kutokana na mikasa yake, ikiwamo kesi ya kumiliki silaha kinyume cha sheria.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
584,000SubscribersSubscribe

Latest Articles