25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Ramires kujiunga na Jiangsu Suning

RamiresNANJING, CHINA

KIUNGO wa kimataifa wa Brazil na klabu ya soka ya nchini England, Chelsea, Ramires Nascimento, anakaribia kujiunga na timu ya Jiangsu Suning ya nchini China.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28, alisajiliwa na Chelsea kutoka Benfica mwaka 2010 kwa pauni milioni 17, wakati huo klabu hiyo kutoka China imeweka mezani kitita cha pauni milioni 25 kwa ajili ya kumnasa nyota huyo.

Ramires alisaini mkataba mpya na klabu yake wa miaka minne Oktoba, mwaka jana, ila alipata nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza katika michezo saba tu msimu huu wa Ligi Kuu nchini England.

Timu ya Jiangsu ilimaliza katika nafasi ya nane katika msimamo wa Ligi msimu wa mwaka 2015, huku kikosi hicho kikiwa kinanolewa na nyota wa zamani wa Chelsea, Dan Petrescu.

Kiungo huyu wa Kibrazil akiwa na The Blues, ametoa mchango mkubwa wa timu hiyo kutwaa mataji mbalimbali kama vile Ligi Kuu, Kombe la FA, ubingwa wa klabu bingwa Ulaya na ile michuano ya Europa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles