28.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

RAIS TRUMP AADHIMISHA SIKU 100 KWA KUKEJELI WANAHABARI

PENNSYLVANIA, MAREKANI


RAIS wa Marekani Donald Trump ameadhimisha siku 100 madarakani kwa kutoa hotuba inayokejeli wanahabari na kutetea mafanikio yake.

Trump aliwaaambia wafuasi wake jimboni hapa juzi kuwa ameridhika kuwa pamoja nao badala ya wanahabari aliopaswa kuhudhuria nao dhifa ya chakula cha jioni.

Imekuwa utamaduni wa muda mrefu kwa Ikulu ya Marekani, kutumia matukio ikiwamo siku 100 za urais madarakani kuhudhuria hafla hiyo maarufu mjini Washington.

Akihutubia umati, Rais Trump amelinganisha na kutofautisha, kile alichotaja 'siku 100 za wanahabari kushindwa na kazi yao', na mafanikio yake aliyodai yametokana na kutimiza ahadi zake kila siku.

Miongoni mwa ahadi hizo alisema ni pamoja na kurejesha ajira za viwanda na kumaliza mzozo katika sekta ya makaa ya mawe.

Pennsylvania ni jimbo linalotegemea uchumi wa uchimbaji madini, na lilikuwa muhimu katika uchaguzi wa mwaka jana.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles