30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Rais Magufuli, Museveni wateta

magufuli na museveniNa Mwandishi Wetu, Arusha

RAIS Dk. John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jana alikuwa na  mazungumzo na Rais wa Uganda, Yoeri Museveni mjini hapa.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilisema  kwa kauli moja, viongozi hao walikubaliana lijengwe bomba la kusafirisha mafuta kutoka Bandari ya Tanga hadi  Uganda.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo,  Rais Museveni alimtembelea Rais Magufuli Ikulu ndogo   Arusha baada ya kuwasili nchini.

Museveni yuko nchini   kuhudhuria mkutano mkuu wa 17 wa kawaida wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  utakaofanyika katika Hoteli ya Ngurudoto  leo.

Akizungumza baada ya mazungumzo hayo ya faragha,  Dk.  Magufuli alisema wamekubaliana kutekeleza mradi  wa bomba la kusafirisha mafuta kutoka Tanga hadi Uganda  kwa manufaa ya nchi zote mbili.

Alisema  bomba hilo litakuwa na urefu wa kilometa 1,120, huku mradi huo ukitarajia kuzalisha ajira ya  watu zaidi ya 15,000.

Rais   Magufuli  alisema pamoja na kujengwa bomba hilo, wamekubaliana kuongeza biashara ndani ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, kujenga viwanda na kuzalisha ajira zaidi.

Alisema katika mkutano unaoanza leo, yatajadiliwa maombi ya   Sudan Kusini kutaka kupata uanachama ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Sudan Kusini ikiwa mwanachama wa jumuiya hiyo itakuwa na uwezo wa kufanya biashara katika eneo lenye takriban watu milioni 150, alisema.

Naye Rais Museveni alimpongeza Rais Dk. Magufuli kwa kasi yake nzuri aliyoanza nayo katika uongozi wake.

Alisema nchi wanachama wa jumuiya hiyo  sasa zitakuwa katika nafasi nzuri ya kwenda na kasi ya   Dk. Magufuli katika shughuli za maendeleo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles