25.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

RAIS MAGUFULI AWAONYA WAKURUGENZI

Anna Potinus

Rais John Magufuli ameagiza kuchukuliwa hatua kwa wakurugenzi wanaowanyima haki zao wafanyakazi kwa kuwahamisha bila kuwalipa posho ya uhamisho.

Ameyasema hayo mkoani Iringa leo katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani, ambayo kitaifa yamefanuika mkoani humo.

“Ukimuhamisha mtumishi mlipe fedha yake kabla ya kumuondoa na hili nalisema kwa mara ya mwisho sitarudia tena kulizungumza hilo katika maisha yangu.

“Leo nimeona bango jingine nafikiri chama cha walimu kinachosema wao wanaendelea kuhamishwa bila kulipwa fedha za uhamisho, najua viongozi wanaosimamia wizara zinazohamisha wako hapa, kama kuna mtu yeyote anahamisha bila kulipa huyo ni jeuri na dawa yake ni kumtoa”, amesema Rais Magufuli.

Pamoja na mambo mengine, Rais Magufuli amewataka wananchi wa Iringa na Njombe kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa Ukimwi kutokana na mikoa hiyo miwili kuongoza kwa ugonjwa huo nchini.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles