27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Rais Buhari ahamaki kuitwa fisadi

Muhammadu_BuhariABUJA, NIGERIA

RAIS wa Nigeria, Muhammadu Buhari, amesema amepigwa butwaa na matamshi ya kushtusha na ya aibu ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron aliyekaririwa akisema Nigeria na Afghanistan ni mataifa fisadi zaidi duniani.

Buhari ameyasema hayo muda mfupi tu baada ya kupata habari hiyo kuhusu kauli zilizotolewa na Cameron.

Akizungumza kupitia msemaji wake, Garba Shehu, ametaja matamshi ya Cameron kuwa ya aibu na kushtua.

“Kiongozi wa Nigeria anasema labda Cameron alikuwa akizungumzia utawala ulioondoka madarakani Mei mwaka uliopita wa aliyekuwa Rais Goodluck Jonathan.

“Buhari alichaguliwa kwa jukwaa la kupambana na ufisadi. Yeye ndiye kifagio cha ufisadi nchini Nigeria.

“Usisahau kuwa Rais Buhari alialikwa katika kongamano la London linalofanyika Alhamisi (leo) kutokana na jitihada zake kubwa za kupigana na ufisadi, itakuwaje awe fisadi,” alisema Shehu.

Habari hizo ziliibuka baada ya Cameron kunaswa na kamera katika dhifa ya kusherehekea miaka 90 tangu kuzaliwa kwa Malkia Elizabeth.

Alisikika akimwambia Malkia, “Viongozi wa mataifa fisadi zaidi duniani wakiwemo wa Afghanistan na Nigeria, yanayoorodheshwa kuongoza kwa ufisadi zaidi kote duniani, watakuwa nchini Uingereza siku ya Alhamisi (leo) kuhudhuria kongamano la kutathmini mbinu za kukabiliana na zimwi la ufisadi.”

Kiongozi wa Kanisa la Anglikana, Askofu Mkuu wa Canterbury, Justin Welby aliyekuwa na viongozi hao wawili anaonekana akimkumbusha Cameron kuwa Buhari aliyeingia madarakani mwaka jana si fisadi.

Hata hivyo Cameron alionekana akiendeleza mada hiyo.

Nigeria pamoja na Tanzania ni nchi pekee kutoka Afrika kati ya nchi 60 duniani zilizoalikwa kuhudhuria mkutano huo wa London.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles