23.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

R. Kelly akubaliwa kuwasiliana na watoto wake

LOS ANGELES MAREKANI

MWANAMUZIKI wa Marekani, Robert Kelly ‘R. Kelly’, kwa sasa ameruhusiwa kuwasiliana na watoto wake, baada ya mke wake wa zamani, Andrea Lee Kelly, kumruhusu kufanya hivyo.

Lee na R. Kelly ni wazazi wa watoto watatu akiwamo, Jay, Joann na Robert Jr,  lakini mwanamuziki huyo alizuiliwa kuwasiliana na watoto wake tangu mapema Desemba mwaka jana, kutokana na tuhuma za ubakaji zilizokuwa zikimkabili.

Lakini Lee, amewaruhusu watoto wake kuwasiliana na baba yao akiamini wamekuwa watu wazima na  kwa sasa wanahitaji mapenzi ya mzazi wao huyo.

“Ni mwezi sasa tangu  mara ya mwisho alipowasiliana na watoto wake, kwa sasa wanaweza kuwasiliana, lakini kamwe siwezi kuwaruhusu watazame dokumenti iliyojaa tuhuma za ubakaji unaomhusu baba yao,” alisema Lee.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles