27.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

POMBE IMEMNILETEA WOLPER UBONGE

Na JESSCA NANGAWE


MWIGIZAJI wa filamu za Bongo, Jackline Wolper, ameweka wazi kwamba pombe ndiyo inayomsababishia unene anaopigania sasa kuupunguza.

Wolper alisema watu wengi wanadhani ulaji wa chakula zaidi ndiyo unaosababisha mwili wake kuwa mnene kiasi cha kutowavutia baadhi ya mashabiki wake lakini ukweli ni kwamba unene huo unasababishwa na unywaji zaidi wa pombe.

“Unajua sikuwa mnywaji na nilikuwa nikiichukia pombe sababu nikinywa ndio napata hamu zaidi ya kula chakula kingi, hivyo kwa sasa nimeanza harakati za kurudisha mwili wangu wa mwanzo uliokuwa ukinionyesha vizuri kwa mashabiki wangu na pia nipo kwenye harakati za kuachana na unywaji wa pombe,” alieleza.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles