30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Polisi wazuia mkutano CUF, wenyewe wagoma

Nora Damian, Dar es Salaam

Mkutano Mkuu wa saba wa Chama cha Wananchi (CUF) upande wa Profesa Ibrahim Lipumba, umeingia dosari baada ya Jeshi la Polisi kuingilia kati na kusema kuna zuio la mahakama.

Mkutano huo unaofanyika leo Jumanne Machi 12, Buguruni jirani na ofisi za chama hicho umeanza asubuhi kwa wajumbe kutoka maeneo mbalimbali nchini kuwasili na wakati zoezi la uhakiki likiendelea, polisi walifika na kuwataka kutoendelea na mkutano huo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Zuberi Chembera, ambaye aliongozana na maofisa kadhaa wa polisi alifika katika ukumbi unakofanyika mkutano huo na kuzungumza na viongozi wa chama hicho wakiwemo Naibu Katibu Mkuu, Magdalena Sakaya na Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano ya Umma, Abdul Kambaya na kuwataka kutoendelea na mkutano.

“Sisi tumeleta taarifa kwamba mkutano una zuio,” alisema Chembera.

Hata hivyo viongozi hao wa Cuf walisema wataendelea na mkutano kwa sababu hawajaona nakala ya maandishi ya zuio hilo.

“Mkutano hauna zuio, je kuna ‘document’ umekuja nayo kamanda….ungekuja nayo tungekuelewa, sisi tunaendelea na mkutano wetu,” alisikika mmoja wa viongozi wa Cuf.

Mwisho.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles