24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

POLISI WAUA WATUHUMIWA WANNE KWA UJAMBAZI

 

Na WALTER MGULUCHUMA- KATAVI

JESHI la Polisi Mkoa wa Katavi, wamewaua watu wanne wanaodhaniwa kujihusisha na ujambazi wakiwa na bunduki mbili za kivita zikiwa na risasi 27.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Benedictor Mapujila, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 5:00 usiku katika eneo la Kahenze, Kata ya Ugala, Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi, baada ya watuhumiwa hao kujibizana na polisi kwa kuwarushia risasi.

“Siku moja kabla ya kuuawa kwa majambazi hao, walimpora mtu mmoja,   Shija Masanja ambaye ni mfanyabiashara simu za Tecno  na fedha taslimu Sh 800,000 na   kutokomea  kusikojulikana.

“Katika msako huo, polisi waliwaona majambazi  hao wakiwa wamejificha kichakani kando ya barabara na baada ya kugundua wanafuatwa na askari walianza kuwafyatulia risasi askari na katika majibizano hayo ya risasi yaliyodumu kwa dakika 15 polisi  waliwaua majambazi wanne na kukamata silaha kadhaa ikiwamo  SMG zenye  namba UA 5538 1997 ikiwa na  risasi 14 kwenye magazine na nyingine yenye namba AFV 0826 1996  ikiwa na  risasi 13 kwenye magazine.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles