31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Pluijm atoa siri ya ushindi

Hans van der Pluijm
Hans van der Pluijm

Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM

KOCHA mkuu wa timu ya Yanga, Hans van der Pluijm, ametoa siri ya ushindi  wa mabao 3-0 dhidi ya African Lyon,  akidai kwamba ulitokana na kuwasoma  kwa  makini wapinzani wao katika mchezo wao wa kwanza waliocheza dhidi ya Azam FC.

Juzi Yanga walianza vema mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, wakifanikiwa kuondoka na ushindi huo mnono katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam juzi baada ya kumalizika kwa mchezo, Pluijm alisema amefurahi kuanza ligi vizuri kwa kupata ushindi mnono.

“Mchezo ulikuwa mgumu kwa pande zote mbili kwani wapinzani wetu walifanya mashambulizi kuhakikisha wanapata ushindi, lakini umakini wa wachezaji wangu ulisaidia kutopata nafasi hizo,” alisema.

Alisema bao la kwanza lilizidisha morali kwa wachezaji wake, ambapo baada ya kufanya mabadiliko kipindi cha pili, walizidisha mashambulizi yaliyopelekea kufunga mabao mengine.

Kocha huyo raia wa Uholanzi, aliongeza kuwa kikosi chake kinazidi kuimarika licha ya kukabiliwa na baadhi ya majeruhi kama Juma Abdul, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Ally Mustafa ‘Barthez’ na Obrey Chirwa.

Pluijm aliendelea kusema atahakikisha anayafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye mchezo huo ili yasijitokeze kwa mara nyingine.

Wakati huo huo, kocha mkuu wa timu ya African Lyon, Bernardo Tavares, amekiri timu yake kutocheza kwa kiwango kizuri kwenye mchezo huo kama ilivyokuwa mchezo uliopita dhidi ya Azam FC.

Tavares alisema kipindi cha kwanza wachezaji wake walikuwa wanacheza kwa kulinda sana lango lao bila kushambulia, hivyo kuwapa mwanya wapinzani wao kupata bao la mapema.

“Mchezo uliopita kikosi changu kilicheza kwa kiwango kizuri sana na kufanikiwa kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Azam FC ila leo (jana), walitengeneza nafasi za kufunga lakini hawakupata bahati ya kufunga,” alisema.

Alisema licha ya kutopata ushindi, anawapongeza wachezaji wake kwa kuendelea kucheza bila kukata tamaa hadi mwisho wa mchezo, akiahidi kwenda kuyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye mchezo huo ili yasijitokeze kwa mara nyingine

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles