26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Obama, Ki-moon watoa hotuba ya mwisho

president-obama-with-un-secretary-general-ban-ki-moon

NEW YORK, MAREKANI

RAIS wa Marekani, Barack Obama  na  Katibu  Mkuu  wa Umoja  wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, wametoa hotuba zao za mwisho katika umoja huo wakiitaka jumuiya ya kimataifa  kuongeza juhudi kukabiliana na mizozo  ya kimataifa.

Waliitaja mizozo hiyo kama kuanzia vita  nchini Syria hadi mgogoro wa  wakimbizi na mpango wa kinyuklia wa Korea Kaskazini.

Aidha, Ki-moon ambaye alihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mara  ya mwisho katika kipindi chake cha  uongozi cha miaka 10, aliwashutumu viongozi  wa  dunia  kwa  kushindwa  kwao  kutatua  mzozo wa  Syria.

Akizungumzia  kuhusu kuvunjika  kwa  mazungumzo  ya amani  katika  Mashariki  ya Kati, Ban  alisema  matumaini ya  suluhisho  la  mataifa  mawili  kati  ya  Israel  na Palestina  yanapungua  siku  hadi  siku kutokana na misimamo mikali hasa ya upande wa Israel.

Wakati huo huo, Rais Obama alitarajia kutangaza msamaha wa madeni na ahadi ya misaada kutoka mashirika  ya Serikali  ya Marekani  na  wawekezaji  binafsi, ikiwa ni sehemu ya juhudi zake kulipatia bara la Afrika nishati.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles