31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

NYONI, NDUDA WATUA SIMBA

Erasto Nyoni

Na THERESIA GASPER-DAR ES SALAAM

SIMBA imeendeleza vurugu zake katika usajili wa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kufanikiwa kuwasajili beki, Erasto Nyoni na kipa  Said Mohamed, huku Yanga ikifanikiwa  kumsainisha mkataba mpya kiungo wake, Thaban Kamusoko.

Nyoni ambaye ni beki wa kulia amemaliza mkataba wake wa kuitumikia Azam FC kama ilivyo kwa Nduda ambaye mkataba wake wa kuichezea Mtibwa Sugar ulimalizika msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Wekundu hao wa Msimbazi, Simba, walikamilisha usajili  wa mikataba ya miaka miwili kwa nyota hao ambao  pia wanaichezea timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ jana baada ya pande zinazohusika kufikia mwafaka.

Nyoni amekuwa akisifika kutokana na uwezo wake mkubwa wa kucheza namba zaidi ya moja na usajili wake unachukuliwa kama tahadhari endapo  beki Shomari Kapombe aliyejiunga pia na timu hiyo akitokea Azam FC hatapona  kwa wakati majeraha yanayomsumbua.

Kwa upande wa Mohammed, anakuwa kipa wa tatu kusajiliwa na Wekundu hao msimu huu baada ya klabu hiyo awali kuwanasa, Aishi Manula kutoka Azam na Emmanuel Mseja aliyesajiliwa akitokea Mbao FC.

Usajili wa makipa hao watatu una maana makipa, Daniel Agyei na Manyika Peter  muda wao wa kuondoka katika klabu hiyo umewadia.

Wakati huo huo, mvutano wa muda mrefu kati ya Yanga na Kamusoko hatimaye umemalizika  baada ya  kiungo huyo wa kimataifa wa Zimbabwe kusaini mkataba mwingine wa miaka miwili.

Wakati huo huo, Singida United imeendelea kufanya yake baada ya jana kufanikiwa kumsajili kipa, Ally Mustapha ‘Barthez’ ambaye amemaliza mkataba wa kuitumikia Yanga.

Mwenyekiti wa Singida United, Festo Sanga, alisema  klabu hiyo imemsajili kipa huyo  ikiamini ataisaidia timu hiyo  kufikisha malengo ya kufanya vizuri katika Ligi Kuu  Tanzania Bara msimu ujao.

“Tumeingia mkataba wa miaka miwili na Barthez, kwani tumeona ana uwezo mzuri wa kuisaidia timu yetu ikafikia malengo ya kufanya vizuri katikia ligi kuu msimu ujao,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles