24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

NMB yazindua huduma ya mikopo ya pikipiki kwa wakazi wa Mwanza

Na  Mwandishi wetu, Mwanza

Benki ya NMB imezindua huduma ya Mikopo ya pikipiki za miguu miwili na miguu mitatu kwa wakazi wa kanda ya ziwa na kuahidi kutumia zaidi ya Sh bilioni 5 kutoa mikopo kwa vijana zaidi ya elfu 75 nchini.

Akizungumza katika uzinduzi wa mikopo hiyo kwa  vijana waendesha bodaboda na bajaji jijini Mwanza, Afisa Mtendaji Mkuu wa benki ya NMB,  Ruth Zaipuna aliwataka wanufaika kujitokeza na kuchagamkia fursa hiyo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB – Ruth Zaipuna akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza – Salum Kalli  muda mfupi baada ya uzinduzi wasmi wa Mikopo ya Pikipiki za miguu miwili na zile za miguu mitatu inayoitwa Mastaboda Loan jiji Mwanza jana. Hafla hiyo ilihudhuriwa na wendesha boda boda zaidi ya 300. Wengine ni Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa Baraka Ladislaus (Kulia Mwisho), Afisa Mkuu wa Rasilimali watu wa Benki ya NMB – Emmanuel Akoonay na Kushoto Mwisho ni Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB – Filbert Mponzi.

Alisema ikiwa vijana na watu wengine waliojiunga katika umoja wa waendesha bodaboda na bajaji watajitokeza na kuchangamkia fursa hiyo, NMB  inaweza kuongeza kiwango cha utoaji mikopo.

Ruth alisema kwa mara ya kwanza walizindua huduma hiyo jijini Dar es Salaam mwezi wa nne mwaka huu na kwamba jana waliingia jijini Mwanza ili kuhakikisha vijana wanatumia fursa hiyo kupata mikopo na hivyo kujiajiri wenyewe.

“Hatutaki mikopo hii iwe mizigo kwenu bali baraka kwenu na  NMB imedhamiria kufika katika mikoa mingine  hapa nchini kwa ajili ya utoaji wa mikopo hii,”‘ alisema Ruth

Afisa Mtendaji huyo wa NMB alisema,  hatua ya utoaji wa mikopo hiyo ni ombi la serikali la kuomba wasaidie vijana kupata mikopo ya bodaboda na bajaji na kwamba wameamua kulitekeleza kwa vitendo.

Kwa upande wake, Mkuu wa kitengo cha wafanyabiashra wadogo wa NMB,  Filbert Mponzi akizungumza katika uzinduzi wa mpango huo, alisema benki hiyo imeandaa mfumo wa malipo  ya  Master Boda QR utakaomuwezesha mteja kumlipa bodaboda nauli.

Alisema ili kupata mkopo wa bodaboda lazima kila mwanachama wa  umoja wa waendesha bodaboda afungue akaunti ya NMB na kuanza kuingiza fedha anayolipwa na wateja kama nauli walau kuanzia miezi mitatu.

Aidha, alisema kila mwezi wanatoa mikopo ya wajasiliamali hapa nchini inayofikia Sh bilioni 40.

Kwa upande mwingine,  aliwaomba Watanzania kujiunga katika vikundi na kufungua bima ya mkono wa pole ambayo itawasaidia wanapopata misiba katika familia zao.

Alisema kiwango cha kila mwanachama katika kikundi anatakiwa Sh. 2000 kwa mwezi na kwamba ikiwa atafariki NMB itatoa Sh. milioni 5.

Aidha, alisema bima hiyo pia itahusisha mwanachama kufiwa na mke  na watoto ambapo pia  NMB  itatoa rambirambi.

Katibu wa waendesha bodaboda mkoani Mwanza, Samue Antony akizungumza katika uzinduzi huo alisema wameweza kuunganisha vijana 100 waliokuwa wakitumia madawa ya kulevya na sasa wamekuwa watu wema ambao wanashirkiana nao.

Aliomba NMB kuendelea kuwapa elimu kuhusu namna bora ya matumizi bora ya fedha watakazopata kupitia vyombo hivyo ili waweze kunufaika.

 Akizindua mpango hu wa mikopo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Salum Kalli aliwahakikishia usalama waendesha bodaboda na bajaji muda wote watapokuwa kazini.

Aidha, aliwataka kuheshimu mikopo watakayopatiwa ili iweze kuwasaidia na kusaaidia makundi mengine ya kijamii  katika jiji la Mwanza na maeneo mengine.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles