25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Nkatha Moses aiweka wazi ‘Umwaminifu’

NAIROBI, KENYA
KUTOKA nchini Kenya, mwimbaji anayekuja kwa kasi, Nkatha Moses, ameweka wazi kuwa wimbo wake mpya, Umwaminifu, umebeba simulizi ya kweli ya maisha aliyopitia.

Akizungumza na MTANZANIA, Nkatha ambaye anasimamiwa na Crosslife Movement, alisema alipata maono ya kuimba wimbo huo kipindi ambacho janga la corona linatikisa Dunia na lengo lake lilikuwa ni kumshukuru Mungu kwa kuwapigania wanadamu.

“Wimbo huu ulitokana na janga na COVID 19 ambalo limesababisha mateso kwa wanadamu ulimwenguni kote pia wakati huo huo baba wa rafiki yangu alikuwa anaumwa yupo ICU, tulimwamini Mungu na uponyaji wake na kweli akatenda.
“Nimeona uaminifu wa Mungu kwa watu wengi hivyo wapendwa wanaweza kuitazama video ya wimbo huu kwenye chaneli yangu ya YouTube naamini watabarikiwa,” alisema Nkatha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles