23 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

NISHATI NYENZO MUHIMU KUPIGANA NA UMASKINI

Na MWANDISHI WETU


WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema nishati ya  uhakika ya umeme itatokomeza umasikini nchini Tanzania ifikapo mwaka 2030.

Profesa Muhongo aliyasema hayo alipokuwa akizindua Jukwaa la Nishati  Tanzania (TEP) pamoja na  mkutano wa siku mbili  kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu, jijini  Dar es Salaam.

Mkutano huo unaolenga kujadili upatikanaji wa nishati endelevu ya kutosha kwa bei nafuu  ya uchumi wa viwanda Tanzania, unakutanisha wadau mbalimbali zikiwemo kampuni za utafiti na uchimbaji wa mafuta na gesi nchini kama vile Statoil, BG na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

 Wadau wengine ni pamoja na kampuni za kuzalisha umeme kama  vile Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Songas pamoja na  mabalozi wa nchi mbalimbali,  taasisi za kifedha na viongozi wa Serikali.

Profesa Muhongo alisema Serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha nishati ya uhakika inapatikana itakayopelekea Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 kama Dira ya Maendeleo ya  Taifa inavyofafanua.

Waziri  Muhongo alisema nishati ya kutosha itapelekea uanzishwaji wa viwanda vidogo hususani katika maeneo ya vijijini na kuzalisha ajira hivyo kupunguza wimbi la vijana kuhamia mijini kutafuta maisha.

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha  Dar es Salaam (UDSM), Florens Luoga, alisema kupitia Jukwaa la Nishati  Tanzania linaloundwa na wataalamu kutoka  Tanzania na Uholanzi, wanaangalia namna ya kushirikiana kupitia kubadilishana uzoefu kupitia programu mbalimbali.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles