24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Nicki Minaj apata mtoto wa kike

 CALIFORNIA, MAREKANI 

MAMA wa rapa Nicki Minaj, Carol Maraj amethibitisha kuwa msanii huyo amejifungua mtoto wa kike mwishoni mwa wiki iliopita. 

Nicki Minaj mwenye umri wa miaka 37, amefanikiwa kupata mtoto huyo wa kwanza na mume wake Kenneth Petty, lakini hakuweka wazi jinsia yake hadi juzi jumapili mama yake alipoamua kuweka wazi kupitia ukurasa wake wa Instagram. 

“Asante sana Mungu kwa kumbariki mwanangu Nicki Minaj na kumpa furaha kubwa, siku zote umekuwa ukinibariki na kuibariki familia yangu. Kwa sasa Nicki umepata baraka kutoka kwa Mungu. 

“Siku zote watoto ni zawadi kutoka kwa Mungu, hivyo tunashukuru kwa kupata ugeni wa mtoto wa kike,” aliandika mama wa Nicki Minaj. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles