25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Nick Cannon kuvuruga ndoa ya Mariah

Hennessy V.S Hosts A Special Dinner With Nick CannonNEW YORK, MAREKANI

RAPA Nick Cannon, ameweka wazi kwamba ana lengo la kutaka kuzuia ndoa na mke wake wa zamani, Mariah Carey, ili asifunge ndoa na bilionea, James Packer.

Cannon alifunga ndoa na mrembo huyo na kufanikiwa kupata watoto wawili mapacha, lakini ilipofika mwaka 2014 wawili hao waliachana na Mariah akapata mchumba mwingine anayetarajia kufunga naye ndoa hivi karibuni.

Rapa huyo amesema bado anampenda Mariah hivyo hayupo tayari kuona mrembo huyo akiolewa na mtu mwingine na yupo tayari kuharibu mapenzi yao.

Rafiki wa karibu na msanii huyo alisema msanii huyo anapanga kuharibu uhusiano wa Mariah na Packer, kwa kuwa bado anampenda mama watoto wake na yupo tayari kurudiana naye.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles