23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Nacte yavifutia usajili vyuo 10

BRIGHITER MASAKI-DAR ES SALAAM

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte) limevifutia usajili vyuo kwa kutokidhi vigezo vya kutoa mafunzo yanayoratibiwa na baraza hilo.

Mkurugenzi wa Uthibiti, Ufuatiliaji na Tathmini, Dk. Geofrey Oleke amesema Baraza limevitaarifu vyuo husika kwa barua juu ya uamuzi huo na kuvitaka kuwahamisha wanafunzi wote kwenda katika vingine vilivyosajiliwa.

Vyuo hivyo ni pamoja na Time School of Journalism Dar es Salaam (TSAJ), ERA Training College Bukoba, Azania College of Management Dar es Salaam, Clever College Dar es Salaam, Aces College of Science (ACES)Mwanakwerekwe, Zanzibar, Zanzibar Institute of Business Research and Technology (ZIBRET), Gender Training Institute, Dar es Salaam.

Oleke amesema vyuo viwili vya College of Business and Management Dar es Salaam na cha Univesity Computing Centre (UCC) Mwanza Campus, viliomba kusitisha mafunzo kwa sababu mbalimbali zikiwemo uwezo wa kifedha wa kugharamia mafunzo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles