24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Nabii: Maovu ya China yamesababisha corona

Na JEREMIA ERNEST

Nabii wa kanisa la Life in Christ Ministry, zoe Prophet Saimon Charisma amesema ameoneshwa kuwa ugonjwa wa corona ulikusudiwa nchi ya China kwa sababu ya maovu yao.

Akizungumza leo na waandishi wa habari amesema ugonjwa huu haukutakiwa kufika Tanzania kwa kuwa haukuletwa kwa sababu yetu.

“Huu ugonjwa ulilenga taifa la China kwa sababu wamemsahau muumba wao, umesambaa nchi nyingine kwa sababu ya hofu ya wanadamu,” amesema.

Ameongeza kuwa anaishukuru serekali kwa kwa kuchukua hatua za tahadhari haraka na kutozuia ibada makanisani ili watu waendelee kumtukuza Muumba.

Aidha amesema ugonjwa huo hauna nguvu hivyo wanachi waondoe hofu na kufuata kanunu na maagizo yanayotolewa na wataalamu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles