Califonia, Marekani
TAASISI ya NAACP, imeweka wazi kuwa itampa tuzo ya heshima (President’s Award), mwimbaji na mwanamitindo, Rihanna Fenty kwenye hafla ya utolewaji wa NAACP Image Awards 2020, huko California, Marekani, Februari 23 mwaka huu.
Katika tuzo hizo ambazo zitatolewa kwa msimu wa 51, huwapa heshima hiyo wasanii au watu maarufu mwenye mchango mkubwa kwa jamii au kuanzisha mambo yenye manufaa kwa jamii.
Mwaka uliopita tuzo hiyo ya heshima alipewa rapa, Jay Z kutokana na mambo kadha wa kadha anayoyafanya kwenye jamii.