24.4 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Mwili wa Kibonde kuwasili leo, kuzikwa Jumamosi

Bethsheba Wambura, Dar es Salaam

Mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa Clouds Media, Ephraim Kibonde, unatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 7, saa nne usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kuzikwa Jumamosi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga, amesema hayo leo wakati akitoa taarifa za msiba huo ambapo amesema mara baada ya mwili huo kuwasili, utahifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.

“Jana usiku niliongea na daktari Derrick aliyekuwa anamtibu Ephraim Kibonde akanihakikishia kuwa anaendelea vizuri lakini bahati mbaya wakati wanaajiandaa kurudi Dar es Salaam hali ikabadilika na kusababisha kifo chake.

“Taratibu za mazishi na maombolezo, zitafanyika kesho nyumbani kwake Mbezi na tunatarajia kuaga na kumpumzisha siku ya Jumamosi,” amesema Kusaga.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles