27 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

MWIGULU: MADEREVA WANAOENDESHA MWENDOKASI WANYANG’ANYWE LESENI

Na Fredy Azzah, Dodoma

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameagiza polisi kumkamata dereva yeyote atakayeonekana anaendesha gari kwa mwendo kasi na asiachiwe hadi atakapofikishwa mahakamani.

Amesema mahakama ikijiridhisha kuwa ni kawaida ya dereva huyo kuendesha kwa mwendo basi dereva huyo anyang’anywe leseni.

“Pia nasisitiza kila basi la abiria liwe na madereva wawili ili mmoja akikamatwa mwingine aendelee na safari,” amesema Mwigulu.

Hatua hiyo imetokana na mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga alioomba kutokana na ajali iliyotokea jana ilisababishwa na shimo barabarani ambapo alitaka Wakala wa Barabara (Tanroads) watozwe faini kwani wamekuwa wakitoza watu faini bila sababu.

Akijibu hoja hiyo, Mwigulu amesema ajali ile haikusababishwa na shimo isipokuwa mwendo kasi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles