27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

MWANASHERIA MKUU TBS AFUTIWA KESI, AKAMATWA

Na PATRICIA KIMELEMETA-DAR ES SALAAM

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemfutia kesi Mwanasheria Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Baptister Bitaho (54), ambaye alikuwa akikabiliwa na mashtaka matatu ikiwamo ya kuishi na kufanya kazi nchini bila ya kuwa na  kibali.

Uamuzi huo umetolewa  na Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa baada ya Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Method Kagoma, kuiomba mahakama kumfutia kesi hiyo chini ya kifungu cha 98(a)cha sharia ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA).

Hata hivyo baada ya mshtakiwa huyo kuachiwa huru, alikamatwa tena na yupo Idara ya Uhamiaji kwa ajili kwa mahojiano.

Awali  Mwendesha Mashtaka wa Uhamiaji, Novatus Mlay alimsomea mashtaka mshtakiwa huyo na kudai kuwa Mei 19, mwaka huu katika maeneo ya Kinondoni kwenye Ofisi ya Uhamiaji, Bitaho akiwa raia wa Burundi alikutwa akiwa  nchini bila ya kuwa na kibali cha mkazi.

Alidai kuwa, siku hiyo  mshtakiwa huyo alikutwa akifanya kazi kama mwanasheria Mkuu wa TBS bila ya kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya kazi hapa nchini.

Alidai kuwa, Julai 6 mwaka 2011 katika Ofisi ya Uhamiaji ya Dar es Salaam iliyopo wilaya ya Ilala, mshtakiwa huyo akiwa raia wa Burundi alitoa taarifa za uongo kuhusu maelezo yake binafsi wakati akijaza fomu ya kuomba hati ya kusafiria namba CT (5)(Ai).

Wakili Mlay aliieleza mahakama hiyo kuwa, kitendo hicho cha kutoa taarifa za uongo kilimuwezesha mshtakiwa huyo  kupata hati ya kusafiria ya Tanzania yenye namba AB 474856 huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za nchi.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, mshtakiwa huyo alikana mashtaka huku upande wa jamhuri ukidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles