25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mwanamuziki wa Marekani kutua nchini Julai

Antique Davis EdutainmentNA GLORY MLAY

MWANAMUZIKI kutoka Oakland, California nchini Marekani, Antique Davis Edutainment, anatarajia
kufanya ziara ya kimuziki Julai nchini Tanzania na Hispania ambapo atatumia wiki tatu.

Mwanamuziki huyo anayeimba muziki Afro pop, Afro Beat, Reggae na Dancehall, aliliambia MTANZANIA kwamba ziara yake itaanzia nchini Ghana ambapo atatumia wiki sita kisha Tanzania na Hispania atakapotumia wiki tatu.

Katika maandalizi ya kutangaza albamu yake mpya ya ‘Remember Vol. II’ anayotarajia kutoa Juni huku asilimia kubwa ya muziki wake ukiwa umeandaliwa nchini Ghana na nchi nyingine za Afrika Magharibi.

“Kiukweli nashukuru kwa nchi za Afrika kutokana na asilimia kubwa ya muziki wangu kuandaliwa huko na sasa nina ziara ya kimuziki kwa ajili ya kutangaza albamu yangu hiyo nimepanga kutembelea, DC&Ghana na Tanzania na kisha nitaelekea Hispania,” alisema Antique.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles