24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mwanamke aliyekabiliwa na uraibu wa ngono, kujichua

Mwanamke aliyekabiliwa na uraibu wa ngono, kujichua NASHAMI Wangara (38), maaru­fu kwa jina la Florence, ni mzaliwa wa magharibi mwa Kenya, ambaye ameamua kuandika kitabu kuhusu maisha yake na kukipa jina la “My Sto­ry for his Glory.” (Hadithi yangu kwa Utukufu wake).

“Nilipokuwa msichana mdogo nilikuwa mnyenyekevu na si­kujua mambo mengi kuhusu maisha, lakini nilipofikisha miaka 18 mambo yalibadilika,” anasema.

Anaongeza kuwa wakati mwingine alikuwa anatoroka nyumbani na kure­jea asubuhi hadi siku moja ambapo mama yake mzazi alipomwambie aam­ue moja kama kuendelea kuishi naye au kuondoka, ambapo msichana huyo aliamua kuondoka.

Anasema alianza uhusiano wake wa kimapenzi wa kwanza na mwana­mume na hatimae akaanza kuishi naye pindi alipoondoka nyumbani kwao.

Haikuchukua muda mrefu, uhusi­ano hu ulianza kukumbwa changamo­to, hali iliyosababisha waachane baada ya kushindwa kusuluhisha tofauti zao.

Hatua hiyo anasema ilimuathiri. ‘’Niliamua kutojiingiza katika uhusi­ano wa kimapenzi na mtu mmoja,’’ anasema.

Akiwa na umri wa miaka 21 akaamua kuwa kila wakati atakuwa na wapenzi zaidi ya wawili ili mmoja akimuudhi awe na wengine.

Na hapo ndipo alianza kutekwa na uraibu wa ngono.

‘’Nilianza kama mchezo kwa kuwa nilikuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume zaidi ya wawili,’’ anasema Nashami.

Anasema ilikuwa rahisi kutimiza matamanio yake kwa kuwa ni kitu ali­chohitaji kufanya kila wakati alipoku­wa na mpenzi wake.

Kwa muda wa miaka sita, alika­biliwa na hali ya kufanya ngono kama uraibu. Ukombozi wake kwa ngono kati ya mume na mke.

Aliamua kuokoka baada ya kuvuti­wa na huduma ya uimbaji na uadilifu wa watu walioimarisha imani yao kidi­ni. Lakini kwa sababu dini ya Kikristo hairuhusu ngono nje ya ndoa, alijikuta akiingia kwenye uraibu mpya wa ku­piga punyeto.

‘’Nilikuwa naweza kujipiga punye­to kama mgonjwa aliyeandikiwa dawa na daktari, asubuhi mbili jioni mbili,” anasema Nashami.

Alikuwa mmoja ya waimbaji wa kwaya kanisani na hali hiyo ilimfanya ajihisi mchafu na asiyekuwa na dha­mana.

Ni tabia ambayo yeye mwenyewe hakuipenda na kila mara ilimfanya ahisi aibu wa kwa kuwa mateka kwa miaka kumi.

Anasema alibadilika baada ya ku­pata maombi maalum. Pia alikuwa anaandamana na watu ambao hawa­kumhukumu bali walimpatia mawaid­ha ya jinsi ya kuondokana na hali hiyo.

Anasema kuwa siyo rahisi kujion­doa katika uraibu wa ngono na puny­eto, lakini inawezekana.

Kwa sasa anawahamasisha vijana kutojiingiza katika hali kama yake.

Mtazamo wa ngono na ponyeto kama uraibu kimatibabu ni upi?

Mwanasaikolojia, Cate Mathea, ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Uraibu wa Ngono, anasema njia rahisi ya kugundua kuwa mtu ametekwa na uraibu huo ni kutathmini maongezi yake.

Kichochezi kikuu anasema ni mawazo ya mtu kuwa kwenye masuala ya ngono na jinsi ya kujichua.

“Kupiga punyeto sio tabia mbaya lakini mtu anapoifanya kila wakati na inapokuwa tu ndicho kitu mtu ana­chokifikiria kila mara kila wakati ina­geuka na kuwa uraibu,” anasema.

Daktari Mathea anasema punyeto hutumiwa zaidi na vijana wanapovun­ja ungo kama njia ya kuondoa ule msu­kumo wa kawaida wa mwili.

Anasema homoni aina ya estrogen huwa kwa mwili wa kila binadamu, kusaidia katika shughuli za ngono kwa watu wazima.

‘’Homoni ya estrogeni ikiwa nyingi mwilini, mtu anakuwa na hamu ya kufanya ngono kupita kiasi,’’ anasema mtaalamu huyo.

Anaongezea kuwa hali hiyo hu­dhibitiwa kwa dawa ambazo mtu hu­pewa ili kupunguza nguvu ya homoni ya estrogen mwilini.

Unawezaje kujiepusha na uraibu wa ngono?

Mwanasaikolojia Cate Mathea, anashauri watu kutotazama filamu za ngono kila wakati.

Pia anasema asilimia 80 ya watu wanaokabiliwa na uraibu wa ngono ni wale ambao walidhulumiwa kingoni wakiwa watoto wadogo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles