30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

MWALIMU WA KIROHO INDIA AFUNGWA JELA MAISHA KWA UBAKAJI

DELHI, INDIA


MAHAKAMA ya Jimbo la Rajasthan nchini India jana imetoa adhabu ya kifungo cha maisha jela dhidi ya mwalimu maarufu wa kiroho Asaram Bapu kwa kumbaka msichana aliyekuwa mfuasi wake mwaka 2013.

Hukumu dhidi ya Bapu (77) ilisomwa ndani ya gereza moja la mji wa Jodhpur, jimbo la Rajasthan kutokana na hofu kuwa wafuasi wake huenda wakafanya vurugu.

Kesi hiyo ni ya karibuni katika mfululizo wa kesi kubwa za ubakaji nchini India ambazo zimesababisha maandamano ya umma na kuzusha maswali kuhusu namna polisi inavyozishughulikia kesi hizo.

Agosti mwaka jana, mwalimu mwingine maarufu wa kiroho, D.k Saint Gurmeet Singh Ram Rahim Insan, alihukumiwa miaka 20 jela kwa mashitaka ya kuwabaka wanawake wawili wafuasi wake.

Bapu amekanusha mashtaka hayo na anaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo katika Mahakama ya Juu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles