23 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Mwalimu Mkuu ampiga mwanafunzi ngumi za uso

boy-bullied

Na MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM

MWALIMU Mkuu wa Shule ya Sekondari Ridhwaa Seminary iliyopo wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, Yusuph Kivugo, amemshambulia mwanafunzi wake, Mbaraka Mwalimu, kwa kumpiga ngumi usoni na kumsababishia maumivu makali.

Mwanafunzi huyo anayesoma kidato cha nne katika shule hiyo iliyopo Kinondoni Mkwajuni, alikutwa na mkasa huo Novemba 3, mwaka huu wakati akijiandaa na mtihani wa Historia.

Kwa mujibu wa ratiba ya mitihani ya taifa ya kidato cha nne inayoendelea nchini, mtihani huo ulikuwa unafanyika mchana, lakini hata hivyo hakufanya kutokana na maumivu aliyokuwa nayo.

“Tulikuwa msikitini na wenzangu tunasoma, ilikuwa ni saa mbili asubuhi kabla ya mtihani wa Historia kuanza, mwalimu alikuja akauliza kwanini tunapiga kelele na kuanza kutupiga.

“Upande wa pili kulikuwa na wanafunzi wa pre-form one ndio waliokuwa wakipiga kelele, nilishangaa kamkunja mwenzangu anaitwa Mohamed akawa anampiga mangumi, mimi nilijua labda kuna kosa amefanya.

“Katika kujitetea akina Mudy walikimbia, mara akaja kwangu akanishika akaanza kunishambulia, amenipiga ngumi nyingi za usoni, kwenye taya na nyingine jichoni kiasi kwamba sikuweza kufanya mtihani kwani jicho lilivimba sana,” alisema.

Mwalimu wa nidhamu shuleni hapo, Omary Ikome, alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Alisema jukumu lake ni kusimamia nidhamu kwa wanafunzi na kwamba suala hilo lipo juu ya uwezo wake.

“Nilimkuta Mbaraka analia na jicho la kushoto limevimba, nilimuuliza akasema amepigwa na mkuu. Mimi nasimamia nidhamu kwa wanafunzi, lakini kwa kuwa kitendo hiki kimefanywa na bosi wangu, siwezi kuzungumzia zaidi kwani lipo juu ya uwezo wangu,” alisema.

Mwalimu mkuu huyo alipoulizwa kiini cha tatizo, hakuweza kutoa ushirikiano na kumfukuza mwandishi ofisini kwake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles