24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Mvua yasababisha maafa Kenya

 NAIROBI, KENYA

KARIBU watu 12 wamepoteza maisha kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya maeneo ya Kenya.

Mshirikishi wa eneo la Bonde la Ufa, George Natembeya alisema watu sita wakiwemo maofisa wawili wa polisi, wamefariki katika maporomoko ya udongo yaliyotokea kwenye mpaka wa kaunti za Pokot Magharibi na Elgeyo Marakwet kufuatia mvua kubwa zilizonyesha usiku wa Jumamosi hadi Jumapili.

Kadhalika watu wengine sita wameripotiwa kufariki dunia katika eneo la Chesogon kauti ya Pokot Magharibi kutokana na mafuriko, mbali na mamia ya familia kuachwa bila makazi.

Habari zaidi zinasema kuwa, kuna watu kadhaa ambao hawajulikani walipo kutokana na mafuriko hayo, huku timu za uokoaji zikiendelea kuwatafuta kando ya Mto Chesogon.

Aidha wakazi wa eneo hilo wametakiwa kuhamia nyanda za juu na kwenye maeneo salama ili kuepusha maafa zaidi kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika eneo hilo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles