26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

MUSUKUMA ATAKA VITI MAALUMU VYA DARASA LA SABA BUNGENI


Na Fredy Azzah, Dodoma  |  

Mbunge wa Geita vijijini, Joseph Kasheku maarufu Musukuma (CCM), ameitaka serikali irudishe kazini watumishi wa darasa la saba iliowafukuza vinginevyo wabunge wenye elimu ya darasa la saba pia waondolewe bungeni.

Musukuma amesema hayo bungeni Mjini Dodoma leo Ijumaa Aprili 6, alipokuwa akichangia hotuba ya ofisi ya Waziri Mkuu.

Amesema wabunge wakishaondolewa bungeni warudishwe kwa Viti Maalumu kama ilivyo kwa wanawake na walemavu ili wawatetee darasa la saba wenzao.

Musukuma amesema hotuba ya Waziri Mkuu inaonyesha mwaka wa fedha uliopita waliojiunga na darasa la saba ni milioni mbili na walioingia sekondari ni 500,000 jambo linalomaanisha wenye elimu ya darasa la saba ni zaidi ya asilimi 80.

“Serikali isiposikia kilio chetu na kuwarudisha kazini watumishi hao na wabunge wa kambi zote kuungana na kutetea watumishi hao waliofukuzwa kazi basi tutakutana 2020,” amesema Musukuma.

 
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles