27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Mufti Zuberi alazwa Muhimbili

Sheikh-Abubakar-Zuberi-bin-AllyNa Veronica Romwald, Dar es Salaam

MUFTI wa Tanzania,   Sheikh Abubakary Zubeir Bin Ali, amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa   matibabu.

Awali MTANZANIA lilipata taarifa kuwa Mufti angefikishwa hospitalini hapo saa 10 jioni na   kulazwa katika jengo la Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).

Mwandishi wa habari hii alifika hospitalini hapo na kwenda moja kwa moja katika jengo hilo ambako mmoja wa madaktari wa zamu ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini alithibitisha taarifa za kulazwa kwa Sheikh Mkuu.

“Tumepokea taarifa hiyo ya kuja kulazwa Mufti kwa ajili ya matibabu na tayari tumeandaa mahali pa kumlaza lakini bado hatujampokea.

“Ili aje kwetu lazima apitie kwanza kwa wenzetu wa emergence (kitengo cha wagonjwa wa dharura) halafu daktari wetu ataenda kumuona ndipo atahamishiwa huku JKCI,” alisema.

Kutokana na majibu hayo, mwandishi   alikwenda kupiga kambi katika eneo la wagonjwa wa dharura ambako baadaye alimshuhudia Mufti Zuberi akiwa ameongozana na baadhi ya ndugu na waumini wa dini ya Kiislamu.

Alipotafutwa, Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Neema Mwangomo hakupatikana katika simu zake wala ofisini kwa kuwa alikuwa katika mapumziko ya mwisho wa wiki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles