26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Mtoto wa Wiz Khalifa aanza kuimba

Amber Rose and Wiz Khalifa pick up SebastianNEW YORK, MAREKANI

MTOTO wa msanii wa hip hop nchini Marekani, Wiz Kharifa, Sebastian ameanza kuonyesha kuwa mtoto wa nyoka ni nyoka baada ya kumshangaza baba yake kwa kuimba wimbo wa ‘See You Again’.

Wimbo huo umezidi kumpa umaarufu msanii huyo, lakini mtoto huyo mwenye umri wa miaka mitatu, alimshangaza baba yake kutokana na uwezo wa kuimba aliouonesha.

“Hiki ni kipaji cha hali ya juu, sijawahi kumuona mwanangu akiimba nyimbo zangu hii ni mara ya kwanza, lakini nimewahi kumuona akisikiliza muziki mara kwa mara, kutokana na uwezo huu ninaamini atakuja kuwa msanii hatari miaka ya baadaye,” aliandika Wiz Kharifa kwenye akaunti ya Instagram.

Hata hivyo, msanii huyo aliweka video ya mtoto huyo kwenye akaunti hiyo, ambapo baada ya kutwa moja kukatika tayari ilikuwa imetazamwa na zaidi ya watu 150,000 na kuikubali.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles