28.6 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 19, 2024

Contact us: [email protected]

MTOTO WA JAY Z APATA TUZO BET

 LOS ANGELES, MAREKANI 

MTOTO wa rapa Jay Z, Blue Ivy Carter, amekuwa mmoja kati ya wale waliochukua tuzo za BET nchini Marekani usiku wa kuamkia juzi. 

Blue Ivy Carter mwenye umri wa miaka nane, ameanza kufuata nyayo za wazazi wake Jay Z na Beyonce, baada ya kuchukua tuzo hilo ikiwa ni msanii aliyeshirikishwa kwenye wimbo wa mama yake ambao unajulikana kwa jina la Brown Skin Girl. 

Wimbo huo wa Beyonce umewashirikisha wasanii wengine kama vile WizKid na SAINt JHN, hivyo wasanii wote walioshiriki kwenye wimbo huo wanahusika kwenye tuzo hiyo. 

Hii sio tuzo ya kwanza kwa wimbo huo, tangu umeachiwa umefanikiwa kuchukua tuzo zingine kama vile 2019 BET Soul Train na 2020 NAACP Image Awards. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
584,000SubscribersSubscribe

Latest Articles