31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

MPAKA WA KILOLO, IRINGA KUAMULIWA NA WATAALAMU

NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula

Na FRANCIS GODWIN -IRINGA

NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula, amepiga marufuku wananchi kutumia eneo lenye mgogoro kati ya Kijiji cha Ilambilole Wilaya ya Iringa na Irole Wilaya ya Kilolo hadi hapo watakapotuma wataalamu kubainisha mpaka unaotenganisha wilaya ya Kilolo na Iringa.

Mbali ya kuzuia kutumia eneo hilo, Waziri Mabula, amemzuia mmoja kati ya  wafugaji wa jamii ya Maasai kuendelea na ujenzi wa nyumba katika eneo hilo huku akiliagiza Jeshi la Polisi wa wilaya hizo kuchukua hatua kali kwa yeyote  atakayepuuza agizo hilo.

Alisema mpaka wowote lazima useme ni  gazeti gani la Serikali lilitangaza katika  mipaka ya Kilolo na Iringa ambayo  ilizaa Kilolo waliweka GN yao namba  366 ya mwaka 2002 hivyo mipaka hiyo ndiyo inayotambuliwa na si vinginevyo.

“Mbali na utambuzi wa mipaka hiyo ni marufuku kwa mtu yeyote kuendelea na shughuli yoyote iwe ya ufugaji, kilimo ama ujenzi katika eneo hilo hadi wataalamu watakapobainisha mipaka hiyo.

“Iwapo kama mpaka wa wilaya na  wilaya hauna tatizo, iweje kuwe na mgogoro wa mipaka ya kijiji wakati mipaka ya wilaya  ipo  sawa, naomba kusema mwananchi wa Kilolo kulima  eneo la Iringa ama mwananchi wa Iringa  kulima ama  kufanya shughuli zake  katika Wilaya ya Kilolo si tatizo na huwezi sema ni mgogoro, mtu anaweza  kulima ama kufanya shughuli zake  popote pale ili mradi asivunje sheria,” alisema Mabula.

Awali  Mbunge  wa Kilolo,  Venance  Mwamoto,  alimweleza  Naibu  Waziri   huyo kuwa wananchi  wa Irole  ndio ambao wana uhitaji mkubwa wa eneo hilo na ndiyo sababu  wamefika katika mkutano huo tofauti na wenzao wa  Ilambilole.

“Siku zote mgogoro huo ni wa pande mbili ila katika hilo inaonyesha  wananchi wa Ilambilole hawana  shida na eneo hilo isipokuwa mtu mmoja kulitaka kwa manufaa yake,” alisema Mwamoto.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles