23.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Morales asema yuko tayari kurejea nchini mwake

LA PAZ, BOLVIA

RAIS wa zamani wa Bolivia, Evo Morales amesema yuko tayari kurejea nchini mwake haraka iwezekanavyo, wakati wafuasi wake wakikabiliana na polisi dhidi ya kiongozi aliyejitangaza mwenyewe Jeanine Anez.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Mexico City, Morales ametaka kufanyike mazungumzo baina ya pande zote, na kusema atarejea nchini endapo ataombwa na watu wake.

Watu wawili walipoteza maisha katika ghasia baina ya wafuasi wa rais huyo na serikali ya muda, sambamba na vikosi vya usalama.

Idadi jumla ya watu waliouawa sasa imefikia 10 wakati wa wiki tatu za maandamano.

Mabomu ya kutoa machozi yalifyatuliwa hapo juzi mjini La Paz, wakati wa maandamano ya kutaka rais huyo wa zamani kurejeshwa madarakani.

Morales alikuwa rais wa Bolivia kwa miaka 13 na alikimbilia uhamishoni siku ya Jumanne na kuchochea makamu wa rais wa Seneti Anez kujitangaza rais.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles