27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Monalisa: Maigizo ya jukwaani ndiyo mkombozi wa filamu za Bongo

Yvone Cherry ‘Monalisa’
Yvone Cherry ‘Monalisa’

Na YASSIN ISSAH, DAR ES SALAAM

WAIGIZAJI wakongwe kwenye tasnia ya filamu nchini Tanzania, Yvone Cherry ‘Monalisa’ na mama yake mzazi, Suzan Lewis ‘Natasha’, wamesema sanaa za jukwaani zitasaidia kipindi hiki ambacho soko la filamu linaonekana kuyumba.

Waigizaji hao walioanza kuigiza jukwaani muda mrefu, walisema hayo baada ya kushirikishwa katika igizo la ‘Mrs Lucy goes to Africa’ lililoonyeshwa juzi katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini hapa.

“Tumefurahi sana kushirikishwa katika igizo hili maana kwa muda mrefu hatukufanya maonyesho kama haya ya uigizaji wa ‘live’ hasa kutokana na soko la filamu kuyumba kwa sasa, hivyo uigizaji wa jukwaani utasaidia kukuza soko hilo kwa mara nyingine,” alifafanua Monalisa.

Naye mwandaaji wa onyesho hilo, Tousant Duchess maarufu Lady T, alisema nia ya tamasha hilo ni kuweka utofauti wa usawa wa burudani ndani na nje ya Tanzania kupitia maonyesho ya jukwaani.

“Nimeanza na Tanzania kisha nitafuata nchi nyingine, pia naipenda nchi hii kwa kuwa ina vipaji vingi lakini pia nitawatangazia wengine huko waje kujionea vipaji vilivyopo hapa,” alisema Lady T.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles