25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

MO FARAH ANYAKUA MEDALI YA SITA YA DHAHABU

London, England

MWANARIADHA wa Uingereza, Mo Farah, juzi jioni alishinda medali ya sita ya dhahabu katika mashindano ya riadha ya dunia yanayoendelea England.

Farah (34), alianza vizuri mashindano hayo yaliyoanza juzi, licha ya kukabiliwa na tuhuma za matumizi ya dawa za kuongeza nguvu, hali iliyochangia kutoonekana katika vyombo vya habari.

Lakini Farah aliweka yote hayo pembeni na kuonesha kiwango safi kilichochangia ushindi wake mnono.

Ushindi huo umekuja baada ya miaka mitano kupita kwa nyota huyo kushinda mwaka 2012, wakati Uingereza ilipokuwa mwandaaji wa mashindano ya Olimpiki.

Akizungumza na mtandao wa BBC, Farah alisema: “Ulikuwa usiku mzuri kwangu, kwa kufanya jambo bora zaidi, haikuwa rahisi kushinda kutokana na ubora wa wapinzani wangu. Ni ushindi maalumu kwangu, pamoja na familia yangu.”

Farah pia alishinda katika michuano ya mwaka 2011, 2013 na 2015, na kukamilisha ndoto yake ya kuwa mtu muhimu kwa taifa lake pamoja na wanariadha wachanga.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles