24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Mnorway asema muziki wa Bongo Fleva hauna ubora

prodyuza Carl HovindNA HERIETH FAUSTINE

PRODYUZA wa muziki kutoka Norway, Carl Hovind, amesema muziki wa Bongo Fleva hauandaliwi kwa ubora ndiyo maana unashindwa kuchezwa kwenye redio za Ulaya.

Carl alisema wasanii wengi wamewekeza kwenye video na kudharau audio za nyimbo zao ndiyo maana hazichezwi nchi zenye maendeleo katika muziki.

“Tatizo kubwa nililoliona Tanzania wasanii wanatumia fedha nyingi hata dola 20,000 kwa ajili ya kuandaa video za nyimbo zao nchini Afrika, lakini audio hawazigharamii,” alisema Carl.

Mtayarishaji huyo ambaye yupo nchini katika studio ya Diamond Platnumz, anatarajia kufanya kazi na wasanii wakubwa na wadogo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles