28.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mlimani City yakumbwa na mafuriko

Mlimani_City,_nordlig_inngangNa Jonas Mushi, Dar es Salaam

MVUA kubwa iliyonyesha Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana   imesababisha maji kuingia na kujaa ndani ya jengo maarufu la maduka ya biashara la Mlimani City lililopo pembezoni mwa barabara ya Sam Nujoma.

MTANZANIA ilifika eneo hilo na kushuhudia maji yakiwa yametuama na kujaa katika maduka mbalimbali likiwamo duka kubwa la Nakumat, Duka la Sumsung na benki ya KCB Tawi la Mlimani City huku wafanyakazi wa jengo hilo wakihangaika kuyatoa nje kwa kuyachota.

Mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya KCB, alisema mvua hiyo ilisabababisha maji kujaa katika eneo ambalo ujenzi unaendelea, lililopo pembezoni mwa jengo hilo na baadaye maji hayo yaliingilia mlango wa nyuma uliopo karibu na benki hiyo.

Alisema maji hayo yamesababisha athari kubwa kwa benki hiyo ikiwamo kuungua  baadhi ya vifaa vya umeme na kuchelewesha muda wa kufungua benki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
584,000SubscribersSubscribe

Latest Articles