28.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Mkoa wa Pwani kutumia bil 25/- ujenzi wa barabara

Na GUSTAPHU HAULE, KIBAHA

WAKALA wa Barabara Mkoa wa Pwani (Tanroads), umepanga kutumia  Sh bilioni 25.4 kutoka katika mfuko wa barabara kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara katika bajeti ya   mwaka 2019/20 .

Mapendekezo hayo yalitolewa juzi na Meneja wa Tanroads Mkoa wa Pwani, Yudas Msangi,katika kikao cha bodi ya barabara kilichofanyika mjini Kibaha chini ya  Mwenyekiti wake Assumpter Mshama ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha.

Akiwasilisha bajeti hiyo, Msangi alisema katika fedha hizo,Sh Shbilioni 10.8 zitatumika katika matengenezo ya barabara kuu zaidi ya kilomita 528, madaraja madogo 84 na daraja kubwa moja na Sh bilioni 14.6  zitatumika katika matengenezo ya barabara za mkoa.

Alisema  kwa barabara za  mkoa  zina urefu wa  kilomita 1009 .70 , madaraja madogo 45 na madaraja makubwa manane, zimepangwa kufanyiwa matengenezo kwa kiwango cha changarawe  ya kawaida na muda maalumu, matengenezo ya kawaida ya lami na matengenezo ya muda maalum ya lami.

Alisema  bajeti hiyo  imezingatia uhalisia na mahitaji ya matengenezo ya barabara za Mkoa wa Pwani na kwamba amewaomba wajumbe wa kikao hicho kushirikiana kwa pamoja   kuhakikisha mpango huo wa bajeti unafanikiwa kama ilivyopangwa.

 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Ramadhani Maneno, aliitaka Wakala wa Ujenzi Tanzania (Tanroads) na Wakala wa Barabara Vijijini (Tarura), kuhakikisha wanawalipa fidia wananchi ambao maeneo yao yamewekea alama ya kubomoa.

Maneno alitoa mfano barabara ya Makofia –Mlandizi –Mzenga kuwa wananchi wa maeneo hayo wamewekewa alama ya X muda mrefu  kwa kuwataka waondoke maeneo hayo kwa kupisha barabara lakini cha ajabu mpaka sasa  wananchi hao hawajalipwa fidia.

Naye Mshama alisema  suala la barabara ni jambo muhimu  kwa sababu  bila kuwa  na barabara nzuri hakuna maendeleo.

Aliwaomba Tanroads na Tarura kufanyakazi kwa ufanisi  kuweza kufikia malengo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles