23.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Mkali wa Iringa amchana Nay wa Mitego

Emanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.
Emanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.

NA RAYMOND MINJA, IRINGA 

MSANII anayefanya vyema katika muziki wa kizazi kipya kutoka Iringa,  Junaisaty Daimond (Junay), amesema anaendelea kushangazwa na mkali wa hip hop nchini, Emanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, kutokuomba radhi hadi leo kwa wasanii na mashabiki wa wasanii aliowatukana katika wimbo wake wa ‘Shika Adabu yako’.

Msanii huyo alisema kitendo cha kuwasema vibaya wasanii wenzake ndicho kinachoshusha muziki wa Nay wa Mitego kwa kuwa hajali heshima kwa wenzake na maisha ya watu wanaomzunguka kwa ujumla.

Msanii huyo anayetamba na wimbo wake wa ‘Changanyachanganya’, alisema kila mtu ana maisha yake aliyoyachagua kuishi ili mradi hamkeri mtu na kwamba  hakuna haja ya kumdisi au kumdhalilisha mwingine  kwa kuwa tu una sehemu ya kusemea .

Junay alisema licha ya msanii huyo kuwa na jina kubwa katika medali ya muziki, yampasa kuomba radhi kwa kuwa aliwaudhi wasanii hao pamoja na mashabiki wao.

“Kumekuwa na tabia ya wasanii kuwasema wenzao vibaya kupitia muziki au watangazaji wanaowafahamu, ni vyema kila mmoja aheshimu uhuru na mawazo ya mtu kwani kila mtu ana haki ya kuishi jinsi anavyotaka ili mradi havunji sheria za nchi,” alieleza msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles