25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

MIRIAM ODEMBA: JIFUNZENI MISINGI YA UREMBO

Na KYALAA SEHEYE


MWANAMITINDO wa kimataifa, Miriam Odemba, amesema warembo wanaoingia kwenye fani ya urembo hawajui misingi ya fani hiyo ndiyo maana wanafanya mambo ya ajabu yanayoaibisha fani hiyo.

“Wakati sisi tunaanza tulifuata nyayo za wanamitindo na warembo waliowika dunia akiwemo Naomi Campbell na tuliangalia mema yake ambayo yanatusaidia hadi leo kuendelea kujitunza na kuendeleza fani hii kwa mafanikio tofauti na mabinti wa sasa ambao wengi wao huingia kwa mkumbo bila kujifunza misingi ya fani hiyo,” alieleza Odemba huku akidai kama misingi hiyo haitafuatwa hakutakuwa na warembo bora kwa miaka mingi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles