30.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Miracolo wasambaza upendo kwa kuchunguza afya ya kinywa bure

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Hospitali ya Miracolo iliyopo Tabata Sanene inasherehekea Sikukuu ya Wapendanao kwa kutoa huduma ya uchunguzi wa afya ya kinywa na meno bure.

Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Dk. Anna – pendo Deogratias, amesema huduma hizo zilizoanza kutolewa Februari Mosi zitaendelea hadi Februari 28 na kuwataka wananchi wajitokeze kuchangamkia fursa hiyo.

Wafanyakazi wa Hospitali ya Miracolo wakionyesha ishara ya upendo kusherehekea Sikukuu ya Wapendanao.

Dk. Anna amesema mwitikio ni mkubwa na kwamba wamebaini watu wengi wana matatizo ya kinywa na meno lakini hawajui.

“Wengi wanakimbilia kung’oa kumbe meno mengine sio ya kung’oa, yanaweza yakatibiwa yakazibwa,” amesema Dk. Anna.

Katika hatua nyingine hospitali hiyo pia imetoa msaada wa vifaa mbalimbali katika Gereza la Segerea kama sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Wapendanao.

Msaada huo ni pamoja na magodoro, sabuni na pampasi ambapo Dk. Anna amesema waliamua kuwasaidia watu walioko kwenye mazingira magumu kwa kuwasambazia upendo.

“Kuna watu wako kwenye mazingira magumu kama walioko gerezani wanatamani kupendwa, mbali ya kuwa na mpendwa wako uliyenaye karibu jaribu kufikiria na jamii nyingine…tuwasaidie wenzetu walioko kwenye mazingira magumu kwa kuwasambazia upendo,” amesema.

Amesema hospitali hiyo pia inatoa huduma mbalimbali za madaktari bingwa kama vile wa watoto, magonjwa ya ndani kama vile moyo, kisukari, presha, mfumo mzima wa chakula, magonjwa ya kina mama na vipimo vyote vya maabara.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles