23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Minaj afanya maandalizi ya ndoa yake

nicki-minaj-meek-millNEW YORK, MAREKANI

MSANII wa hip hop nchini Marekani, Nicki Minaj, ameweka wazi sehemu ambayo atafunga ndoa na mpenzi wake Meek Mill, mwaka 2016.

Wasanii hao wamekuwa kwenye uhusiano kwa mwaka mmoja sasa, hivyo wanatarajia kufunga ndoa mwakani huku Minaj tayari akiweka wazi sehemu sahihi ambayo wataifungia ndoa hiyo.

“Mwaka 2016 ninatarajia kufunga ndoa na Meek Mill, ninaona sehemu sahihi ya kufungia ndoa hiyo ni kanisani au ufukweni.

“Sehemu zote mbili ziko tayari lakini muda ukifika itaeleweka wapi ni sehemu sahihi ya kufungia ndoa yetu,” alisema Minaj.

Wawili hao walivishana pete Aprili mwaka huu na kuweka wazi kwamba 2016 watakamilisha kila kitu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles