31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

MIAMALA SIMU ZA MKONONI YAINGIZA TRILIONI 13/-

Na ESTHER MNYIKA-DAR  ES SALAAM


 

Semu MwakyanjalaKAMPUNI za simu za mkononi zimejipatia Sh trilioni 13.07 kupitia miamala ya huduma za fedha katika kipindi cha miezi miwili.

Fedha hizo zimepatikana kwa njia ya mitandao katika   miezi miwili ya Novemba na Desemba mwaka jana.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kaimu Meneja wa Habari  wa Mamlaka  ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Semu Mwakyanjala

alisema fedha hizo zimepatikana kutokana na ongezeko kubwa  la matumizi  ya huduma za fedha kwa njia ya mitandao ya simu  nchini.

Alizitaja kampuni zilizohusika na miamala hiyo kuwa ni   Zantel kupitia huduma ya (Easy Pesa), Tigo (Tigo pesa), Vodacom (Mpesa), Airtel (Airtel Money na Halotel (Halopesa).

Mwakyanjala hakufafanua  Serikali imepata kiasi gani cha kodi kutokana na fedha hizo za miamala pamoja na kiasi ambacho kila kampuni imejipata kutokana na mzunguko wa fedha hizo kwa njia ya mtandao.

“Mwezi Novemba tulikusanya Sh trilioni 6.47 na Desemba Sh trilioni 6.60, jumla ya makusanyo yote kwa miezi hiyo miwili ni wastani wa Sh trilioni 13.07 kupitia miamala ya simu za mkononi.

“Asilimia kubwa ya mzunguko wa fedha  hupitia kwenye simu za mkononi kwa sababu watu wengi hivi sasa wanafanya miamala kwa njia ya mitandao ya simu kwa kutuma, kupokea fedha na kulipia huduma mbalimbali za umeme, maji na nyinginezo,”alisema Mwakyanjala.

Mwakyanjala aliwatahadharisha wananchi  kuwa makini  na matapeli wanaoghushi utaratibu wa mawasiliano kwa kuwalaghai watu kutuma fedha kupitia simu za mkononi.

Alisema katika siku za karibuni, matapeli hao wamekuwa wakituma ujumbe mfupi wa maandishi ambao unaonyesha mtu ametumiwa fedha kwa makosa na baadaye kufuatiwa na ujumbe mwingine unaofanana na ule wa watoa huduma ambako muhusika hutakiwa kurudisha fedha hizo.

“Nawashauri wananchi wasitekeleze maagizo yoyote kutokana na ujumbe wa simu za mkononi unaohusu fedha kwa mawasiliano ya simu.

“Hata kama inatoka kwenye namba ya mtu anayemfahamu, mpigie aliyekutumia ujumbe kwa namba nyingine  kufanya uhakiki,” alisema Mwakyamjala.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles