27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Mgonjwa aliyechubuka ngozi ya mgongo aomba msaada

AMON MTEGA-SONGEA

MKAZI A wa Mtaa wa Kibulang’oma Manispaa ya Songea, Mwajuma Mfaume (23), ameiomba Serikali na wadau mbalimbali kumsaidia kupatiwa matibu ya maradhi ya kuugua mgongo ambao unakidonda kikubwa miaka miwili sasa.

Akizungumza na MTANZANIA  mjini hapa jana, alisema maradhi hayo yalimkuta Septemba, 2017 saa 8 usiku akiwa amelala chumbani kwake.

Alisema akiwa amelala, alijisikia mgongo unawaka moto na alipoamka na kuugusa alikuta ngozi yote imenyofoka, huku akisikia maumivu makali.

 Alisema baada ya tukio hilo, mama yake mzazi Fatuma Bashiru alimpeleka Hospital ya Misheni Peramiho ambako alitibiwa bila kupata mafanikio ya ugonjwa huo  na hatimaye wakamrudisha nyumbani.

Alisema wakiwa  nyumbani, walishauriwa na majirani waende Hospitali ya Rufaa ya ya Mkoa wa Ruvuma na walipofika walianza tena matibabu ambapo kidonda kilikuwa kikisafishwa kwa gharama ya  Sh 45,000, lakini  mwisho wa siku walishindwa kumudu garama hizo kutokana na kidonda hicho kutokuonyesha dalili za kupona.

“Nina maumivu makali, nalala kifudifudi muda wote, mama yangu anapata taabu namna ya kunihudumia,nimeambiwa kidonda kioshwe kwa dripu la maji ambalo hugarimu shilingi  2,500 kila baada ya siku moja,fedha hizi mama yangu hana ,maana ana mzigo mkubwa wa kuniuguza mimi,”alisema.

Mama mzazi Fatuma, alisema amehangaika na mwanaye kufanikisha matibabu kwa kuomba misaada mbalimbali, lakini hajafanikiwa .

Alisema waliwahi kupata kibali cha Ofisa Mtendaji wa Kata ya Lizaboni kilichotolewa Novemba 27, mwaka huu apite kuomba fedha  kwa wafanyabiashara wa maduka jambo ambalo alishindwa kutokana na kukosa muda wa kufanya hivyo.

Katika hatua nyingine, aliwaomba a watu wenye kuguswa na hali ya mwanae basi waweze kumtafuta kwa namba ya simu ya kiganjani ,0653-543498.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles