29.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Meya wa jiji kuikumbuka Dar kwa mashairi

Isaya Mwita
Isaya Mwita

NA TUNU NASSOR, DAR ES SALAAM

MASHINDANO ya mashairi yatakayofanyika Julai 30 na 31, mwaka huu katika viwanja vya Karimjee jijini hapa yamelenga kukumbuka historia ya Jiji la Dar es Salaam ambalo lilisifika kwa ushairi na tenzi nzuri.

Mwandaaji wa mashindano hayo, mstahiki Meya wa jiji hilo, Isaya Mwita, alisema mashairi hayo yataghaniwa na wazee wa jiji hilo ambapo watawakilisha mada mbalimbali katika tenzi zao.

“Tungependa watukumbushe historia ya Mzizima ilikuwaje, Mwalimu Julius Nyerere alipoingia Dar es Salaam walimpokeaje na kwanini maadili ya vijana yanamomonyoka,” alisema Mwita.

Pia Meya huyo aliongeza kwamba Septemba 23 na 24, mwaka huu kutakuwa na maonyesho ya utalii wa ndani ambapo ngoma kutoka makabila mbalimbali ya Tanzania zitaonyeshwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles